• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 8:55 PM
Real Madrid wapepeta Getafe na kufungua pengo la alama 12 kileleni mwa jedwali la La Liga

Real Madrid wapepeta Getafe na kufungua pengo la alama 12 kileleni mwa jedwali la La Liga

Na MASHIRIKA

REAL Madrid walifungua mwanya wa alama 12 kileleni mwa jedwali la Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) mnamo Jumamosi usiku baada ya kucharaza Getafe 2-0 ugani Santiago Bernabeu.

Miamba hao walifungua ukurasa wa mabao katika dakika ya 38 kupitia kwa Casemiro aliyejaza kimiani krosi ya Vinicius Junior kabla ya Lucas Vazquez kufunga goli la pili aliposhirikiana na Rodrygo.

Sasa wanajivunia alama 72 huku mgongo wao ukisomwa kwa mbali na Sevilla. Barcelona wanashikilia nafasi ya tatu kwa pointi 57 sawa na mabingwa watetezi Atletico Madrid waliokomolewa 1-0 na Mallorca.

Real walitamalaki mchezo na kumiliki asilimia kubwa ya mpira huku wakielekeza Getafe makombora 26. Fataki ya pekee iliyotatiza kipa Thibaut Courtois wa Real kati ya nane zilizofyatuliwa na Getafe ni ya Enes Unal iliyobusu mwamba wa goli katika kipindi cha pili.

Ushindi wa Real unatarajiwa kuwapa motisha zaidi kadri wanavyojiandaa sasa kumenyana na Chelsea katika marudiano ya robo-fainali ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) mnamo Aprili 12, 2022 uwanjani Bernabeu. Real wanaonolewa na kocha Carlo Ancelotti watashuka dimbani wakijivunia ushindi wa 3-1 katika mkondo wa kwanza ugani Stamford Bridge.

MATOKEO YA LA LIGA (Jumamosi):

Mallorca 1-0 Atletico Madrid

Real Madrid 2-0 Getafe

Cadiz 1-0 Real Betis

Villarreal 1-1 Bilbao

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Neymar na Mbappe waongoza PSG kusagasaga Clermont ligini

KIGODA CHA PWANI: Kingi atikisa siasa za Kilifi na Mombasa...

T L