• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 1:05 PM
Neymar na Mbappe waongoza PSG kusagasaga Clermont ligini

Neymar na Mbappe waongoza PSG kusagasaga Clermont ligini

Na MASHIRIKA

NEYMAR na Kylian Mbappe walifunga mabao matatu kila mmoja katika ushindi wa 6-1 uliosajiliwa na Paris Saint-Germain (PSG) dhidi ya limbukeni Clermont katika Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) mnamo Jumamosi usiku.

Ushindi huo wa PSG uliwasaidia kufungua mwanya wa alama 15 kati yao na nambari mbili Rennes kileleni mwa jedwali.

Wawili hao waliwapa waajiri wao uongozi wa 2-0 chni ya dakika 20 za kipindi cha kwanza kabla ya Jodel Dossou kurejesha Clermont mchezoni kunako dakika ya 42. Penalti ya Neymar na bao jingine kutoka kwa Mbappe yalifanya mambo kuwa 4-1 kufikia dakika ya 74.

Mbappe ambaye ni raia wa Ufaransa alipachika wavuni goli la tano la PSG katika dakika ya 80 kabla ya Neymar kuzamisha kabisa chombo cha wenyeji wao dakika tatu baadaye.

Lionel Messi alichangia mabao matatu yaliyofungwa na PSG ugani Gabriel-Montpied.

PSG sasa wanajiandaa kwa gozi kali la ‘Le Classique’ litakalowakutanisha na Olympique Marseille mnamo Aprili 17, 2022.

MATOKEO YA LIGUE 1 (Jumamosi):

Clermont 1-6 PSG

Reims 2-3 Rennes

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Simanzi watu sita wakiangamia Murang’a baada ya moto...

Real Madrid wapepeta Getafe na kufungua pengo la alama 12...

T L