Na MASHIRIKA
NEYMAR na Kylian Mbappe walifunga mabao matatu kila mmoja katika ushindi wa 6-1 uliosajiliwa na Paris Saint-Germain (PSG) dhidi ya limbukeni Clermont katika Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) mnamo Jumamosi usiku.
Ushindi huo wa PSG uliwasaidia kufungua mwanya wa alama 15 kati yao na nambari mbili Rennes kileleni mwa jedwali.
Wawili hao waliwapa waajiri wao uongozi wa 2-0 chni ya dakika 20 za kipindi cha kwanza kabla ya Jodel Dossou kurejesha Clermont mchezoni kunako dakika ya 42. Penalti ya Neymar na bao jingine kutoka kwa Mbappe yalifanya mambo kuwa 4-1 kufikia dakika ya 74.
Mbappe ambaye ni raia wa Ufaransa alipachika wavuni goli la tano la PSG katika dakika ya 80 kabla ya Neymar kuzamisha kabisa chombo cha wenyeji wao dakika tatu baadaye.
Lionel Messi alichangia mabao matatu yaliyofungwa na PSG ugani Gabriel-Montpied.
PSG sasa wanajiandaa kwa gozi kali la ‘Le Classique’ litakalowakutanisha na Olympique Marseille mnamo Aprili 17, 2022.
MATOKEO YA LIGUE 1 (Jumamosi):
Clermont 1-6 PSG
Reims 2-3 Rennes
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO