Na MASHIRIKA
MADRID, Uhispania
REAL Madrid imepanga kufanya usajili wa nguvu kwenye dirisha la usajili la majira ya kiangazi ili kurudisha makali ya klabu hiyo pale Bernabeu.
Rais wa klabu hiyo Florentino Perez amesema kwamba katika mipango hiyo, Madrid inataka kuwanasa Kylian Mbappe, Erling Haaland na Paul Pogba kwa ajili ya msimu ujao wa 2022/23.
Perez amewapa maajenti wake ruhusa ya kuanza kuwatafuta mastaa hao, na tayari kuna madai kwamba tayari wameanza kuwasiliana nao.
Madrid walikosema kidogo kumnasa Mbappe lakini sasa watampata kama mchezaji huyu dirisha hilo la usajili litakapoanza rasmi, pamoja na Pogba iwapo wachezaji hao watakuwa hawajapewa mikata mipya kwenye klabu zao za sasa PSG na Manchester Uinted.
Bosi huyo anaamini kwamnba ujio wa nyota hao utaifanya timu yake kuwa moto wa kuotea mbali kwenye ligi kuu ya La Liga na mashindano mengine yoyote.