• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 8:50 AM
Sadio Mane kuadhibiwa kwa kumlima ngumi Leroy Sane

Sadio Mane kuadhibiwa kwa kumlima ngumi Leroy Sane

NA MASHIRIKA

MUNICH, Ujerumani

MSHAMBULIAJI raia wa Senegal Sadio Mane anakabiliwa na hatari ya kuadhibiwa vikali na klabu yake ya Bayern Munich.

Hiyo ni baada ya video kuibuka akimlima ngumi mchezaji mwenza Leroy Sane kufuatia kichapo cha 3-0 dhidi ya Manchester City kwenye Klabu Bingwa Ulaya, Jumanne.

Mawinga hao walionekana wakibijazana wakitoka uwanjani Etihad baada ya kipenga cha mwisho kulia.

Inasemekana mambo yaliharibika walipoingia katika chumba cha timu kubadilisha mavazi. Mane anaaminika alikerwa na alivyoongeleshwa na Sane na akarushia Mjerumani huyo ngumi usoni. Wawili hao walitenganishwa, huku Sane akisalia na jeraha la mdomo. Mabingwa wa Ujerumani, Bayern bado hawajazungumzia suala hilo, ingawa ripoti zinasema kuwa wachezaji hao watakutana na viongozi wa klabu hiyo kutafuta amani.

Ripoti zinadai kuwa viongozi wa Bayern Munich Oliver Kahn na Hasan Salihamidzic wamezungumzia adhabu Mane anafaa kupokea. Vyombo vya habari Ujerumani vinasema kuwa Mane, 31, pia anatarajiwa kuomba msamaha.

“Adhabu zinazoangaliwa ni pamoja na faini, kupigwa marufuku na hata kutengwa kutoka kikosini,” ripoti zimesema.

Aidha, viongozi Paris Saint-Germain wanatumai kuwa na huduma za masupastaa wao Kylian Mbappe na Lionel Messi dhidi ya nambari mbili RC Lens kwenye Ligue 1, Jumamosi.

Wawili hao walirejea mazoezini Jumatano. Kocha Christophe Galtier alikuwa amefichua kuwa Mbappe na Messi walioshiriki mchuano dhidi ya Nice Jumamosi iliyopita, walikuwa na jeraha.

  • Tags

You can share this post!

JURGEN NAMBEKA: Heko Mwadime kutimua wafisadi ila uozo...

Pombe haramu, mitambo ya kamari yaharibiwa Juja

T L