• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
Shujaa yatiwa kundi la kifo Dubai Sevens

Shujaa yatiwa kundi la kifo Dubai Sevens

Na GEOFFREY ANENE

KENYA Shujaa imetiwa katika kundi ngumu la Raga za Dunia duru ya Dubai Sevens ambalo liko na miamba Australia, Afrika Kusini na Great Britain.

Droo ilifanywa Jumapili usiku baada ya Australia kutoka chini na kulima Fiji 20-17 katika fainali ya Hong Kong Sevens ambapo Shujaa ya kocha Damian McGrath ilivuta mkia kwenye ligi hiyo ya mataifa 16.

Kenya, Afrika Kusini, Great Britain na Australia wako Kundi A. Fiji, Argentina, New Zealand na Uruguay walitiwa katika Kundi B nao Ufaransa, Ireland, Uhispania na mabingwa wa Afrika Uganda wako Kundi C. Kundi D linaleta pamoja Samoa, Amerika, Canada na Japan.

Duru ya Dubai Sevens ni Desemba 2-3. Itafuatiwa na Cape Town Sevens mnamo Desemba 9-11 kabla ya duru za Hamilton (New Zealand), Sydney (Australia), Los Angeles (Amerika), Vancouver (Canada), Hong Kong (Hong Kong), Singapore (Singapore), Toulouse (Ufaransa) na London (Uingereza) mwaka 2023.

Australia inaongoza msimu 2022-2023 kwa pointi 22 ikifuatiwa na Fiji (19), Ufaransa (17), Samoa (15), Argentina (13), Amerika (12), Ireland (10), Afrika Kusini (10), New Zealand (nane), Canada (saba), Great Britain (tano), Uhispania (tano), Uruguay (tatu), Japan (mbili) na Kenya mkiani (moja).

You can share this post!

Raila apinga sera za serikali ya Ruto

Tiba rahisi za nyumbani kwa mzio wa ngozi na vipele

T L