Na MASHIRIKA
MSHAMBULIAJI Son Heung-min alifunga bao lake la 100 katika EPL na kusaidia waajiri wake Tottenham Hotspur kutandika Brighton 2-1 katika uwanja wao wa nyumbani.
Bao jingine la Spurs lilijazwa kimiani na nahodha Harry Kane ambaye sasa ana magoli 25 msimu huu, huku Brighton wakifutiwa machozi na Lewis Dunk.
Son, ambaye ni raia wa Korea Kusini, sasa ndiye sogora wa kwanza kutoka bara Asia kuwahi kufunga mabao 100 katika EPL. Ushindi dhidi ya Brighton ulisaza Spurs katika nafasi ya tano kwa alama 53, tatu nyuma ya Manchester United nan a Newcastle United. Brighton wanashikilia nafasi ya saba kwa pointi 46, moja nyuma ya nambari sita Aston Villa waliopepeta Nottingham Forest 2-0.
MATOKEO YA EPL (Jumamosi):
Man-Utd 2-0 Everton
Aston Villa 2-0 Nottm Forest
Brentford 1-2 Newcastle
Fulham 0-1 West Ham
Leicester 0-1 Bournemouth
Tottenham 2-1 Brighton
Wolves 1-0 Chelsea
Southampton 1-4 Man-City
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO