• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 3:09 PM
Stoke City wakomesha rekodi ya kutoshindwa kwa West Brom kwenye Championship

Stoke City wakomesha rekodi ya kutoshindwa kwa West Brom kwenye Championship

Na MASHIRIKA

NICK Powell alifunga bao la pekee katika ushindi wa 1-0 uliowezesha Stoke City kupiga breki rekodi ya kutoshindwa kwa West Bromwich Albion katika Ligi ya Daraja ya Kwanza nchini Uingereza (Championship).

Chini ya kocha Michael O’Neill, Stoke City waliwazidi West Brom maarifa katika takriban kila idara huku Jacob Brown na Mario Vrancic walishuhudia makombora yao yakigonga mwamba wa goli la West Brom.

Wawili hao walimwajibisha vilivyo kipa Sam Johnstone aliyefanya pia kazi ya ziada kwa kudhibiti fataki za Sam Surridge aliyepoteza penalti.

Ilikuwa hadi dakika ya 79 ambapo Stoke City almaarufu The Potters walipata bao la ushindi ambalo kwa mujibu wa kocha Val Ismael wa West Brom, wenyeji wao walistahili kufunga ikizingatiwa ubora waliodhihirisha uwanjani.

Ushindi huo uliosajiliwa na Stoke mbele ya mashabiki 22,703 wa nyumbani, uliwapaisha hadi nafasi ya tatu kwenye msimamo wa jedwali la Championship

  • Tags

You can share this post!

Pep Guardiola akiri kwamba Jurgen Klopp amemfanya kuwa...

Williams Inaki wa Bilbao aweka rekodi ya kuchezeshwa katika...