• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
Thika Queens kujipanga upya tayari kwa kampeni za msimu

Thika Queens kujipanga upya tayari kwa kampeni za msimu

Na JOHN KIMWERE

THIKA Queens imepania kurejea kivingine kwenye kampeni za Ligi Kuu ya Soka ya Kenya (KWPL) muhula ujao.

Meneja wake Glenston Muganda amedokeza hayo baada ya kampeni za msimu uliyokamilika wiki iliyopita.

Thika Queens ya kocha, Benta Achieng inalenga kufanya usajili wa nguvu kuchochea wenzao kwenye kampeni za kusaka ubingwa wa taji hilo ililobeba msimu uliyotangulia.

”Inahitaji tujipange vizuri ili kubeba taji la msimu ujao baada ya kuteleza na kushindwa kuhifadhi taji la msimu uliyokamilisha mapema mwezi huu,” meneja huyu amesema na kuongeza kuwa washika dau wa soka nchini wanastahili kuwekeza zaidi kwenye soka ya wanawake.

Alidokeza kuwa kampeni za msimu huo zilishuhudia ushindani mkali kinyume na ilivyotarajiwa.

Ikiwa imesalia mechi nne meneja huyu alinukuliwa akisema kuwa walipania kumaliza pengine katika nafasi ya pili kwenye jedwali la ngarambe hiyo.

Meneja huyu ametaja baadhi ya wachezaji muhimu waliosaidia klabu hiyo kwenye mechi za msimu uliopita kama Lydia Waganda, Juliet Andibo, Stella Odhiambo, Wincate Kinyua, Mishi Mbaru na Wendy Achieng.

Kwenye mechi ya mwisho Thika Queens ilitoka nguvu sawa bao 1-1 dhidi ya Wadadia FC na kumaliza ya nne kwa kuzoa alama 36, sawa na Zetech Sp.

  • Tags

You can share this post!

Vipusa wa Tausi wazidi kujinoa tayari kushiriki Kipute cha...

Kingi hafai kumlaumu Raila, asema Mung’aro

T L