• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 8:50 AM
Ulinzi Starlets imani tele taji lao

Ulinzi Starlets imani tele taji lao

Na JOHN KINWERE

KOCHA wa Ulinzi Starlets, Joseph Mwanza amejaa imani kuwa wamekaa vizuri kutwaa taji la Ligi Kuu ya Soka ya Wanawake Kenya (KWPL) muhula huu.

Kocha huyo amesema hayo baada ya timu hiyo kupambana kufa kupona na kubeba taji la pili tangu ijiunge na kipute hicho. Ulinzi chini ya nahodha Neddy Atieno imetwaa taji la Super Cup kwa kutungua malkia wa mchezo huo nchini Thika Queens kwa mabao 9-8 kupitia mipigo ya matuta wa kawaida.

”Haikuwa mteremko bali ilibidi tupambane kiume ili kuzima wapinzani wetu. Tulikuwa tumejiandaa kuwakanbli vilivyo maana pia wao sio wepesi,” kocha huyo alisema na kuongeza wapo tayari kupigania ubingwa wa Ligi Kuu.

Hilo ni taji la pili kwa Ulinzi Starlets baada ya kutwaa kombe la FKF Womens ilipocharaza Vihiga Queens mabao 2-1. Naye kocha wa Thika, Benta Achieng alilaumu marefarii na kusema ”Waamuzi wa mchezo huo hawakuzingatia sheria za mpira vizuri lakini tumekubali yaishe tupatane kwenye mechi za ligi.

” Kwenye patashika ya Super Cup, kipindi cha kwanza timu hizo zilitoka sare tasa. Kipindi cha pili dakika ya 66, Rebbecca Akinyi Okwaro alifungia Thika Queens kabla ya Lucy Nato kusawazishia Ulinzi dakika kumi baadaye.

You can share this post!

FIFA yagonga Gor kiboko cha miaka 2 kwa sababu ya jeuri

Serikali kutumia kila familia Sh3,000 kukabili ukame

T L