• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
VITUKO: Kidosho adai Sanchez ana wivu na Fabinho

VITUKO: Kidosho adai Sanchez ana wivu na Fabinho

IMEKUSANYWA NA CHRIS ADUNGO

REBECA Tavares ambaye ni mke wa kiungo Fabinho Henrique wa Liverpool, amemchemkia fowadi wa Inter Milan, Alexis Sanchez kwa kumchezea mumewe visivyo Jumanne usiku.

Sanchez, 33, alifurushwa uwanjani kwa kadi ya pili ya manjano baada ya kumkabili Fabinho kivoloya kwenye mechi hiyo ya marudiano ya hatua ya 16-bora ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) ugani Anfield.

Japo Fabinho, 28, alikamilisha mchuano huo licha ya kuumia kifundo cha mguu, Rebeca hakumsaza Sanchez – mvamizi wa zamani wa Barcelona, Arsenal na Manchester United aliyewahi kumtaka kichuna huyo kimapenzi.

“Sanchez, mbona univunjie mume? Ama ungali na kinyongo kwa kuwa nilikukataa? Je, hutaki Fabinho aendelee kuniburudisha chumbani?” akaandika kipusa huyo kwenye Instagram na kuchangamsha zaidi ya mashabiki 140,000 anaojivunia kwenye mtandao huo wa kijamii.

Rebeca ambaye ni mwanasoka wa zamani ni shabiki sugu wa Fabinho. Wawili hao walianza kutoka kimapenzi mnamo 2013 kabla ya kula yamini ya ndoa miaka miwili baadaye.

Rebeca alijiunga na timu ya wanawake ya AS Monaco Fabinho akichezea madume wa kikosi hicho cha Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1). Hata hivyo, alistaafu soka pindi Fabinho alipojiunga na Liverpool mnamo Mei 2018.

  • Tags

You can share this post!

NYOTA WA WIKI: Tammy Abraham

TAHARIRI: Adhabu kwa Gor Mahia iwe funzo kwa timu zinazozua...

T L