• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 9:55 AM
Zappacosta aondoka Chelsea na kurejea Italia kuchezea Atalanta

Zappacosta aondoka Chelsea na kurejea Italia kuchezea Atalanta

Na MASHIRIKA

BEKI raia wa Italia, Davide Zappacosta, 29, amekatiza uhusiano wake na Chelsea na kurudi nchini mwake kuchezea kikosi cha Atalanta katika Ligi Kuu ya Serie A.

Nyota huyo aliwahi kuvalia jezi za Atalanta kabla ya kujiunga na Torino mnamo 2015 kisha Chelsea mnamo 2017. Tangu wakati huo, aliwajibishwa na Chelsea mara 26 katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) na akafunga bao moja pekee ugani Stamford Bridge.

Mchuano wake wa mwisho kuchezea Chelsea ambao ni wafalme wa Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) ni ule uliowashuhudia wakipepeta Arsenal kwenye fainali ya Europa League mnamo 2019. Tangu wakati huo, alitumwa kwa mkopo kambini mwa AS Roma na Genoa.

Kocha Thomas Tuchel alikuwa radhi kumwachilia Zappacosta ajiengue ugani Stamford Bridge ikizingatiwa kwamba anajivunia mabeki Cesar Azpilicueta na Reece James ambao viwango vyao ni vya juu zaidi kwa sasa.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

DIMBA PWANI: Nyika Queens FC yatafuta dira upya baada ya...

Aubameyang afunga mabao matatu na kusaidia Arsenal kuponda...