NA BRIAN OCHARO
JOPOKAZI la kutatua mizozo ya vyama vya kisiasa limesimamisha kwa muda uamuzi wa chama cha ODM kumteua Bi Zamzam Mohamed kuwania nafasi ya Mwakilishi wa Kike Mombasa.
Uamuzi huo umetolewa kufuatia malalamishi ya mpinzani wake, Bi Asha Hussein Mohamed almaarufu ‘Ashuu’, ambaye amedai hakutendewa haki. Mwanachama wa jopokazi hilo, Bw Erastus Orina, alisema uamuzi huo utadumu hadi maagizo zaidi yatakapotolewa.
Chama kilifanya kura za mchujo mnamo Aprili 22, ambapo Bi Zamzam alitangazwa mshindi.