• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Gachagua asema kazi yake kubwa ni kuzuia watu fulani kumfikia Rais Ruto

Gachagua asema kazi yake kubwa ni kuzuia watu fulani kumfikia Rais Ruto

NA WINNIE ONYANDO

NAIBU Rais Rigathi Gachagua sasa anadai kuwa kazi yake kuu ni kumchunga Rais William Ruto.

Akizungumza akiwa Kaunti ya Nyeri, Jumamosi (Septemba 9, 2023), mwanasiasa huyo alidai kuwa jukumu lake ni kumchunga Rais Ruto dhidi ya ‘watu waliona lengo la kumwangamiza’ rais.

“Mimi sasa kazi yangu ni kumchunga Rais wetu dhidi ya watu wanaotaka kumwangamiza. Tunamjua sana Bw Raila Odinga. Amekuwa akitatiza mfumo wa kila serikali akiwa ndiye mpinzani mkuu,” akasema Bw Gachagua.

Kadhalika, alisema kuwa lengo lake kuu ni kuhakikisha kuwa Dkt Ruto hasumbuliwi na yeyote.

Kando na hayo Bw Gachagua alisema kwamba ameweka vitego Ikuluni kuhakikisha kuwa kiongozi wa Muungano wa Azimio la Umoja One Kenya hamfikii Rais Ruto.

“Niweweka vitego Ikuluni. Hata kuna watu ambao nimeweka wanipigie simu wakimuona Bw Odinga akikaribia Ikuluni. Hii ni kwa sababu najaribu kumlinda rais wetu dhidi ya Bw Odinga,” akaongeza Bw Gachagua.

Haya yanajiri siku chache baada ya Bw Gachagua kumkaribisha Bw Odinga katika Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa wa Kenyatta (KICC) jijini Nairobi kuhudhuria Kongamano la Afrika Kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi.

Viongozi hao wawili wamekuwa wakishambuliana hadharani huku wakirushiana cheche za maneno.

  • Tags

You can share this post!

Wanaume wawili wazuiliwa kwa kukuza bangi shambani

Mzae bila wasiwasi tupate watu wa kutupigia kura –...

T L