NA WALTER MENYA
NAIBU RAIS WILLIAM RUTO ameita mawaziri watano na Baraza la Magavana kuhudhuria mkutano wa Baraza la Serikali la Bajeti na Uchumi (IBEC) na kuzua wasiwasi kuwa siasa ambazo amekuwa akiendeleza zitazuka kwenye mkutano huo.
Mkutano huo wa Novemba 22 unajiri wakati Dkt Ruto akishutumu baadhi ya mawaziri alioita, na iwapo watafika katika makazi yake rasmi eneo la Karen, Nairobi ambayo amekuwa akitumia kwa kampeni za urais kabla ya uchaguzi mkuu wa2022.
Mawaziri hao wamekuwa wakimlaumu Dkt Ruto kwa kuwalaumu huku wakisema wanafuata maagizo ya Rais Uhuru Kenyatta ambaye ametofautiana na naibu wake.
Kuna hisia huenda akatumia mawasilisho katika mkutano huo kujipigia debe kuhusu uchaguzi wa 2022.
Miongoni mwa mawaziri ambao amealika ni Charles Keter (ugatuzi), Ukur Yattani (Fedha), Prof George Magoha (Elimu), Peter Munya (Kilimo) na James Macharia ( Uchukuzi).
Naibu Rais amekuwa akilalama kuwa maafisa wa serikali wanampigia Raila debe badala ya kuwahudumia Wakenya
Vyama vya kisiasa vyatakiwa kufanya NDC kufikia Februari 2022 ili viwe na muda wa kutosha kuandaa teuzi za watakaowania nyadhifa.