• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 8:55 PM
‘Mawaziri wako huru kuunga Raila mkono’

‘Mawaziri wako huru kuunga Raila mkono’

NA RICHARD MUNGUTI

MADAI ya Naibu wa Rais Dkt William Samoei Ruto ni kwamba mawaziri wanaopigia debe mwaniaji wa urais wa Azimio Raila Odinga wanavunja sheria ikitiliwa maanani wawahudumia Wakenya.

Ingekuwa ni vyema wajitenge kushiriki katika kampeni za kupigia vinara wa miungano ya kisiasa debe lakini hakuna sheria inayowakataza kutoshiriki au kujihusisha na masuala haya ya siasa.

Kifungu nambari 23 (1) cha sheria za maadili kinawaruhusu mawaziri katika serikali kuu na serikali za kaunti kushiriki katika harakati za kampeni.

Sheria hii inawakataza watumishi wengine wa umma kushiriki katika kampeni za kisiasa ama kuunga mkono mwaniaji yeyote wa kiti cha kisiasa.

Pia wamekatazwa kuwa maajenti wa wawaniaji viti vya kisiasa.

  • Tags

You can share this post!

Wataalamu wapendekeza sheria za mifugo zitathminiwe...

TUSIJE TUKASAHAU: Ahadi ya mabwawa Nanyuki imekuwa ni ndoto...

T L