• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 3:09 PM
Nitajitenga na Mudavadi iwapo ataungana na Ruto, Nyaribo asema

Nitajitenga na Mudavadi iwapo ataungana na Ruto, Nyaribo asema

Na RUTH MBULA

GAVANA wa Nyamira Bw Amos Nyaribo, amekashifu kauli ya kiongozi wa chama cha Amani National Congress (ANC), Musalia Mudavadi kwamba ananuia kuungana na Naibu Rais William Ruto.

Haya yanajiri siku mbili baada ya Bw Mudavadi kuzuru Nyamira na kutoa matamshi yaliyochukuliwa kuwa anaweza kuungana na Dkt Ruto.

Jana, Bw Nyaribo alisema hawezi kufuatia yeyote katika chama cha United Democratic Alliance (UDA) ishara kwamba atakataa wadhifa wa Naibu Kiongozi ambao ANC inampatia iwapo Bw Mudavadi ataungana na Dkt Ruto.

Bw Nyaribo amesema kwamba hatakubali wadhifa huo iwapo ANC itaungana na UDA na Dkt Ruto.

“Katika ziara yangu Ikonge leo ambako nilifika katika kanisa la Ikonge PAG na kufanya mkutano mjini Ikonge, niliwakumbusha watu wetu kwamba hatuwezi kuingia UDA,” alisema.

. Ni matumaini yangu kwamba chama changu cha ANC, katika Kongamano lijalo la Wajumbe wa Kitaifa (NDC) Januari 23 kitafanya uamuzi utakaofaidi watu wetu na nchi yetu,” alisema Nyaribo katika ukurasa wake wa Facebook baada ya ziara ya Bw Mudavadi. Aliongeza: “Muhimu kabisa, katika akili yangu,ni wazi kuwa siwezi kuungana na UDA,” akasema.

  • Tags

You can share this post!

Mbadi taabani kuhusu hatima yake ya kisiasa

Idara yaonya kuhusu wahubiri bandia Kilifi

T L