NA RICHARD MUNGUTI
CHAMA cha ODM chazimwa na mahakama kuondoa kwenye rejista jina la Seneta wa Kisumu Prof Tom Ojienda na wabunge wanne; wabunge waliotimuliwa chamani wiki jana ni Felix Odiwuor (Langata), Caroli Omondi (Suba Kusini), Gideon Ochanda (Bondo) na Elisha Odhiambo (Gem).
Mwenyekiti wa Jopo la Kutatua Mizozo ya Vyama vya Kisiasa (PPDT) Desma Nungo ameamuru ODM isifute majina ya wanasiasa hao katika sajili yake.