NA WINNIE ONYANDO
WASHIRIKA wa Naibu Rais William Ruto wamekaidi serikali wakisema hawatakoma kutumia maneno yaliyopigwa marufuku na Tume ya Uwiano na Utangamano wa Kitaifa (NCIC).
Walisema kuwa serikali haitawaelekeza na watayatumia maneno hayo katika hafla zao zote za kisiasa.
Dkt Ruto alianza kukaidi agizo hilo Ijumaa dakika chache baada ya NCIC kutoa tangazo hilo baada ya kutoa wimbo anaoita ‘Hatupangwingwi’ na kuuweka kwenye mtandao wa Twitter.
Kiongozi wa Ford Kenya, Moses Wetangula, mbunge wa Malindi Aisha Jumwa na mwenzake wa Garissa mjini Aden Duale walisema tume hiyo haina mamalaka ya kuunda sheria.