Na MASHIRIKA
ARSENAL walididimiza matumaini yao ya kukamilisha kampeni za Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) msimu huu ndani ya orodha ya nne-bora na hivyo kufuzu kwa soka ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu ujao baada ya Brighton kuwatandika 2-1 mnamo Jumamosi ugani Emirates.
Ilikuwa mara ya kwanza kwa Brighton kushinda mechi baada ya michuano saba iliyopita. Walifungua ukurasa wa mabao kupitia kwa Leandro Trossard kabla ya Enock Mwepu kupachika wavuni goli la pili.
Arsenal ya kocha Mikel Arteta ilirejeshwa mchezoni mwishoni mwa kipindi cha pili kupitia bao la Martin Odegaard. Kikosi hicho sasa kinakamata nafasi ya tano kwa alama 54, tatu zaidi nyuma ya Tottenham Hotspur waliotandika Aston Villa 4-0.
Brighton walipaa hadi nafasi ya 11 kwa pointi 37 sawa na Leicester City na Crystal Palace licha ya kushinda mechi ya nne pekee kati ya 26 zilizopita katika EPL.
MATOKEO YA EPL (Jumamosi):
Everton 1-0 Man-United
Arsenal 1-2 Brighton
Southampton 0-6 Chelsea
Watford 0-3 Leeds
Aston Villa 0-4 Tottenham
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO