• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
Ukusanyaji wa saini za kumng’oa Ruto kukamilika wiki ijayo – Raila

Ukusanyaji wa saini za kumng’oa Ruto kukamilika wiki ijayo – Raila

NA CECIL ODONGO

KIONGOZI wa Azimio La Umoja-One Kenya Raila Odinga ametangaza kwamba mchakato wa kukusanya saini za kumwondoa madarakani Rais William Ruto umeanza na kwamba shughuli hiyo itakamilika wiki ijayo.

Muungano huo unalenga kukusanya angalau saini 10 milioni.

Bw Odinga ambaye amefika katika uwanja wa Kamukunji dakika chache kabla ya saa saba mchana leo Ijumaa, ametoa wito kwa wafuasi wa upinzani na Wakenya kwa ujumla wanaohisi athari mbaya za utawala wa serikali ya Kenya Kwanza wajitokeze kwa wingi saini zao zichukuliwe kukamilisha mchakato huo.

“Nitaanza hapa hapa kuweka saini na nyinyi nyote mtapata karatasi mtaweka saini zenu ili kabla ya mwisho wa wiki ijayo, tuwe na saini zaidi ya milioni 10 za kumwondoa Ruto mamlakani

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Azimio Bw Wycliffe Oparanya ambaye alikamilisha mihula miwili akiwa Gavana wa Kakamega, ameongoza kikosi cha Azimio katika kituo cha magari ya uchukuzi wa umma mjini Mumias kukusanya saini za raia.

Timu ya Azimio eneo la Magharibi imeongoza maandamano katika miji ya Luanda (Vihiga), Sabatia (Vihiga), Mumias (Kakamega), Kitale (Trans Nzoia) na mjini Bungoma (Kaunti ya Bungoma).

  • Tags

You can share this post!

Polisi wakamata waandamanaji 3 Banda Street, wawakanyaga...

Saba Saba: Msafara wa Raila Kamukunji wafurushwa na polisi

T L