NA MAUREEN ONGALA
MCHUJO wa chama cha Pamoja African Alliance (PAA) ulisimamishwa katika baadhi ya vituo baada ya kutokea vurugu, kukiwa na madai ya kuwapendelea baadhi ya wawaniaji.
Wanachama walimtaka kinara wao, Amason Kingi aingilie kati jambo hilo, la sivyo waungane na vyama vingine kunyima wawaniaji wa PAA kura Agosti.
Malalamishi hayo yalitokea baada ya wafuasi wa wagombea kukosa majina yao katika sajili za kupiga kura.
Majina ya baadhi ya wagombeaji pia hayakuwa kwenye karatasi za kupigia kura.