NA KALUME KAZUNGU
WAPIGAKURA katika Kaunti ya Lamu, wamechagua wanaume pekee kuwawakilisha katika Bunge la Kaunti baada ya aliyekuwa diwani pekee mwanamke, Bi Anab Mohamed Haji, kushindwa uchaguzini.
Bi Haji (Jubilee) aliyekuwa akiwakilisha Wadi ya Hindi, alishindwa na Bw James Njaaga wa Chama cha Safina.
Wakati huo huo, madiwani saba kati ya 10 wa Kaunti hiyo walipoteza nyadhifa zao baada ya kushindwa debeni.