DIMBWINI LIKONI
Na DOMINIC MAGARA
TABIA YA MLOFA mmoja kuchungulia madirisha ya watu wakiwa wamelala, imefikia kikomo pale alipogusa waya za stima na kurushwa mbali.
Wakazi wa mtaa huu waliamshwa na kelele usiku wa manane wakidhani walikuwa wamevamiwa na wezi.Kwa mshangao, walimpata kalameni, jirani yao akiwa anagaa gaa kwa maumivu makali na kuomba msaada kupelekwa hospitali. Uchunguzi wa haraka ulibaini kwamba, alirushwa na waya wa stima.
Inadokezwa kwamba, bila kuona aibu wala kusita, alieleza masaibu yake. Alijitambulisha kama mmoja wa makosimeni mtaani, wanaojulikana kwa kuchungulia madirisha ya watu usiku wakiwa wamelala.
Furaha ya kutazama sinema katika nyumba za watu iligeuka kuwa balaa pale alipopata jeraha kubwa na maumivu makali.