Na RICHARD MUNGUTI
MWANIAJI wa mwisho kuhojiwa Ijumaa kutaka kujaza nafasi ya Jaji Mkuu alishangaza maafisa wa JSC aliposema atakuwa akimpigia simu mke wa Rais Uhuru Kenyatta kujua hisia zake, kabla ya kumpigia simu kujadili masuala nyeti ya idara ya mahakama.
“Nitakuwa ninampigia simu mkewe Rais Bi Margaret Kenyatta kujua hisia za (Mzee) Rais Uhuru Kenyatta ndipo nimpigie simu kumueleza changamoto ninazokumbana nazo katika utekelezaji wa kazi yangu kama Jaji Mkuu,” wakili Bi Alice Jepkoech Yano alisema, akijibu maswali.
Alisema masuala kama vile ufisadi, kupotea kwa faili za kesi, mrundiko wa kesi ambao umefikia milioni moja ni miongoni mwa changamoto atazishughulikia endapo atateuliwa.