• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 8:55 PM
Muungano wa kaunti umekufa

Muungano wa kaunti umekufa

Na Barnabas Bii

MUUNGANO wa kiuchumi wa kaunti za Kaskazini mwa Bonde la Ufa (NOREB), uliopigiwa upatu kubadilisha chumi za eneo hilo, sasa unaelekea kufa.

Licha ya kwamba ulibuniwa kuvutia wawekezaji wa kimataifa na wa humu nchini ili kuinua kilimo, muungano huo sasa haupo hai na hata sekretariati yake haitekelezi jukumu lolote.

Imebainika kwamba kaunti saba zilizotia saini mkataba wa kuingia kwenye muungano huo tayari zimejiondoa na kuacha tu Uasin Gishu.

Kaunti hizo ni Samburu, Baringo, Turkana, Nandi, Pokot Magharibi, Trans-Nzoia na Elgeyo-Marakwet.Gavana wa Nandi, Stephen Sang’, alikiri kwamba Noreb inakabiliwa na changamoto za kufaulisha baadhi ya miradi iliyokumbatia mwanzoni kutokana na ukosefu wa kifedha.

Bw Sang hata hivyo, alikanusha vikali kwamba kaunti yake imejiondoa Noreb kutokana na hali kwamba pia ipo katika muungano wa kiuchumi wa kaunti za Ziwa Viktoria (LREB).

Kaunti wanachama wa LREB ni Bomet, Bungoma, Busia, Homa Bay, Kakamega, Kericho, Kisii, Kisumu, Migori, Nandi, Nyamira, Siaya, Trans Nzoia na Vihiga“Bado tupo Noreb kutokana na wazo jumuishi la kuinua viwango vya kilimo na ufugaji.

Hata hivyo LREB ndiyo soko ya mazao hayoya kilimo,” akasema Bw Sang.

You can share this post!

Hazina ya NG-CDF kufadhili elimu ya wanafunzi vyuoni

TAHARIRI: Uhifadhi mazingira usiwe ni siku moja