• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 3:55 PM
Avunja mbavu waumini kuomba pasta idhini ili aoe mke wa pili

Avunja mbavu waumini kuomba pasta idhini ili aoe mke wa pili

NA TOBBIE WEKESA

KHWISERO, MUMIAS

WAUMINI waliohudhuria ibada katika kanisa la hapa waliangua vicheko baada ya polo kurai pasta ampe ruhusa ya kuoa mke wa pili.

Jamaa alipiga moyo konde akanyanyuka kitini wakati wa ibada kueleza masaibu anayopitishiwa na mwanadada aliyemuoa kwa harusi.

“Pasta, nimeona mengi katika ndoa yangu. Mke niliyeoa kwa harusi amenifanyia vituko. Ninaomba ruhusa ya kuoa mke wa pili,” polo akamuomba mchungaji.

Vicheko vilisikika kanisani huku baadhi ya waumini wanaume wakimrai pasta aridhie ombi la jamaa.

“Huyu ndugu anafaa kutuzwa maana ameongea kitu cha maana sana kwa niaba ya wengi wanaoumia kisiri. Si yeye peke yake anahitaji ruhusa hiyo, tuko wengi!” kalameni mmoja alisikika akisema.

  • Tags

You can share this post!

Wakulima waanza kugeukia mitambo ya jadi kuepuka gharama ya...

Wakenya wamtarajia Rais kuangazia shida zao akituhubia...

T L