NA CORNELIUS MUTISYA
MUTITU, MACHAKOS
KIOJA kilishuhudiwa hapa mwanadada alipozushia mumewe akimlaumu kwa kumnyima haki yake ya tendo la ndoa kwa muda mrefu.
Kulingana na mdaku wetu, wawili hao walioana miaka saba iliyopita na wakajaliwa mtoto mmoja wa kiume.
Hata hivyo, ndoa yao ilikuwa ya kisirani maana walikuwa wakigombana kila siku.
Jamaa aliingilia ulevi na akaanza kulala popote bila kujali familia yake. Hilo lilifanya mkewe kuanza kulalamika kwa kuhisi upweke kila siku.
Siku ya tukio, mwanadada alichemka kwa hasira na kumzushia mumewe kwa kumzimia ngono kwa muda mrefu sana.
“Umeniacha katika bahari ya upweke. Kwa nini ulinioa?” aliwaka huku jamaa amenyamaza kimya kabla wote kuingia ndani ya nyumba yao.