NA JOHN MUSYOKI
NTALANI, YATTA
NUSURA mlevi mmoja kutoka hapa azabwe makofi na pasta kwa kumvuruga alipokuwa akihubiri kwenye krusedi.
Krusedi ilianza bila bughudha lakini pasta alipokaribishwa kuhubiri, mlevi mmoja alitoka kusikojulikana na kupanda jukwaani na kumrushia pasta cheche za matusi.
Pasta alimpuuza hadi pale jamaa alipoanza kumnyang’anya kipaza sauti.
“Naomba ushuke haraka kabla nikuzabe makofi. Shindwe pepo mchafu,” pasta alimwambia mlevi huyo.
Pasta aliacha kuhubiri ili kumwondoa jamaa jukwaani.
“Huwezi kunikemea. Mimi si devil,” mlevi aliropokwa.
Ilibidi baadhi ya waliohudhuria krusedi kumtimua jamaa huyo na hali ikatulia.
Subscribe our newsletter to stay updated