• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 12:38 PM
Pasta asitisha injili kutimua jombi aliyesumbua akihubiri

Pasta asitisha injili kutimua jombi aliyesumbua akihubiri

NA JOHN MUSYOKI

NTALANI, YATTA

NUSURA mlevi mmoja kutoka hapa azabwe makofi na pasta kwa kumvuruga alipokuwa akihubiri kwenye krusedi.

Krusedi ilianza bila bughudha lakini pasta alipokaribishwa kuhubiri, mlevi mmoja alitoka kusikojulikana na kupanda jukwaani na kumrushia pasta cheche za matusi.

Pasta alimpuuza hadi pale jamaa alipoanza kumnyang’anya kipaza sauti.

“Naomba ushuke haraka kabla nikuzabe makofi. Shindwe pepo mchafu,” pasta alimwambia mlevi huyo.

Pasta aliacha kuhubiri ili kumwondoa jamaa jukwaani.

“Huwezi kunikemea. Mimi si devil,” mlevi aliropokwa.

Ilibidi baadhi ya waliohudhuria krusedi kumtimua jamaa huyo na hali ikatulia.

  • Tags

You can share this post!

Ushoga: Maaskofu wa Kanisa Katoliki nchini Kenya wamtetea...

Yafichuka ulaghai wa bima hupotezea serikali mamilioni

T L