• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 2:58 PM
Slayqueen aachwa kwa mataa sponsa aliporudi kwa mkewe

Slayqueen aachwa kwa mataa sponsa aliporudi kwa mkewe

NA JANET KAVUNGA

KISAUNI, MOMBASA

MWANADADA aliyekuwa akijigamba kwa kumweka kinyumba mume wa mtu alibaki pweke jamaa aliporudi kwa mkewe.

Demu huyo aliishi kuringia wenzake kwamba hawajui mbinu za kunasa wanaume masonko.

Jamaa alikuwa akitumia maelfu ya pesa kufadhili maisha yao ya anasa.

Wenzake walimuonya aache kuringa na mume wa mtu lakini aliwapuuza akidai wana kinyongo.

Juzi, jamaa aliondoka kwa kipusa na kumtumia ujumbe kumwarifu kwamba amerudia familia yake.

Kisha akampiga bloku ya simu ili demu asijaribu kuwasiliana naye.

Siku hizi kidosho anadandia tuktuk kwenda kazini kinaya na hapo awali wakati sponsa alikuwa akimbeba kwa gari la kifahari.

  • Tags

You can share this post!

Matumaini ya stima kuacha kupotea Kisii washukiwa wa wizi...

Hali tete miili ikianza kuzagaa Gaza huku Israel ikipanga...

T L