NA RICHARD MUNGUTI
AJENTI wa upakiaji na upakuaji bidhaa amekana alimlaghai mfanyabiashara Sh600,000 alizodai ni za kulipia gari ushuru.
Inadaiwa kwamba Stanley Ng’ang’a alimlaghai Bw Ben Anyango Alila pesa hizo kati ya Novemba 1, 2019 na Mei 24, 2021.
Upande wa mashtaka umesema Ng’ang’a alifanya uhalifu huo katika mtaa wa Kilimani, Nairobi.
Shtaka lilisema mshtakiwa alidai angelipia ushuru gari muundo wa Range Rover Sports Car alilomwigizia Bw Alila nchini kutoka ng’ambo.
Bw Alila alifahamishwa Bw Ng’ang’a angemsaidia kulipia gari lake ushuru na kuliondoa katika bandari ya Kilindini kabla ya Novemba 1, 2019.
Bw Alila alizuru afisi za Mamlaka ya Ushuru Nchini (KRA) na kugudua gari lake halikuwa limelipiwa.
Hakimu mwandamizi Bi Monica Maroro alimwachilia mshtakiwa kwa dhamana ya Sh1 milioni.