• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 7:55 PM
Ashangaza kutoa kilemba akiteta Mungu ‘amemuacha’ baada ya kupoteza Sh800 katika kamari

Ashangaza kutoa kilemba akiteta Mungu ‘amemuacha’ baada ya kupoteza Sh800 katika kamari

NA MWANGI MUIRURI

Murang’a Mjini 

MWANAMUME mmoja wa Imani ya Akorino mnamo Jumamosi alitoa kilemba chake akiteta kwamba Mungu alimtaliki ndio maana akapoteza Sh800 katika mchezo wa kamari.

Mwanamume huyo alikuwa amefika katika kibanda kimoja kilichoko katika steji kuu ya Mukurwe-ini ambapo uchezaji kamari huandaliwa kwa saa 24 kwa siku.

“Alipata mchezo ukiwa juu wa bahati nasibu na akaingiwa na tamaa. Alikubali kubahatisha Sh800 zake lakini ikaishia alichoma beti,” akasema mdokezi.

Kwa hasira, polo alifoka kwamba haikuwa haki yeye akiwa mwokovu acheze kamari dhidi ya watu waliokuwa miongoni mwa wavutaji sigara, walevi na waraibu wa tumbaku na miraa na yeye anoe wao wakivuna.

“Ndipo alisema kwamba imani yake ilikuwa imetikiswa pakubwa na hakuwa na nia tena ya kung’ang’ania kukaa katika wokovu wasiokiri ufalme wa mbinguni wakimcheka kwa hasara zake,” ikaarifiwa.

Kwa hasira, alitoa kilemba chake cheupe na akakigonganisha chini huku akiapa kuanza maisha ya anasa za ulimwengu.

“Lakini kuna wapita njia waliomshawishi akome hasira kwa kuwa huenda Mungu alikuwa akimuonya kwamba uchezaji kamari katika danguro hilo haramu ni kinyume cha sheria na badala ya kugadhabika, angepata adhabu hiyo ya tamaa yake kwa unyenyekevu,” akasema shahidi mmoja.

Danguro hilo la uchezaji kamari hutajwa sana kwa kuwa hifadhi ya majambazi wa kila aina giza la Mji wa Murang’a.

Polo alitulia na akachukua kilemba chake, akaomba kwanza kuomba Maulana msamaha na kisha akajifunga tena kichwani huku akionekana kujutia maamuzi yake ya siku hiyo.

 

[email protected]

 

  • Tags

You can share this post!

Mtandao wa bure wazinduliwa katika masoko ya Pwani

Kaunti zatenga pesa chache za bima ya afya

T L