• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 8:55 PM
Barua ya mwisho Joseph Murigi aliandikia mkewe kabla ya kujiua

Barua ya mwisho Joseph Murigi aliandikia mkewe kabla ya kujiua

Na MWANGI MUIRURI

“Kwa wakati mwingine ni sharti ujitoe kafara ndio unayempenda zaidi apate afueni ya kuishi atakavyo.

Bibi wee, uliumiza roho yangu katika hii ndoa yetu kupitia visa vya uasherati. Si mara moja hata uliweka afya yetu wawili taabani kiasi kwamba isipokuwa ni matibabu ya dharura yaliyotuweka kwa madawa kwa miezi sita, tungeangamia.

Lakini sababu nilikupenda, nilikusamehe hayo yote. Hii ni licha ya visa vyako kadha vya uavyaji mimba.

Kila mara uliniacha na kwenda raha na hao uliokuwa ukisaliti mapenzi yangu kwako nao, wakishachoka na wewe, ulikuwa unarejea kwangu na ninakupokea kwa mikono yangu miwili.

Kana kwamba haikuwa makosa, kana kwamba haukuwa umeondoka.

Yaliyonikera zaidi ni uliozama nao kwa huo uasherati wakakuchukua video na picha ukiwa katika kitendo nao na wakanitumia.

Mimi nikakutumia video na picha hizo nikikuuliza ni kwa nini sasa iwe hata wapenzi wako haramu wananidunisha hivyo.

Wewe ulikimbia katika kituo cha polisi cha Sabasaba na ukanishtaki eti mimi ndiye nilikuwa nazisambaza video na picha hizo mitandaoni.

Ukisaidiwa na maafisa wako wafisadi, mlijaribu hata kuniua mkiniitisha hongo. Afisa mmoja ambaye pia ni muasherati mwenzako akanikamata, akanipeleka mahali na kunitesa kwa masaa matano akinidai hongo.

Mwishowe katika kituo cha Sabasaba ulifanikiwa kudai fidia kutoka kwangu na masalio ulikuwa upate kutoka kwangu.

Mimi nilikutunza, nikakuvalisha, nikakulisha, nikakulipia karo na nikalisha familia yako katika unyonge wao.

Nakuandikia ujumbe huu kukwambia kwaheri nikisonga kujitoa kafara ili kudhihirisha mapenzi yangu kwako licha ya ukatili huo wako kwangu.

Familia yangu ambayo ni baba na mamangu wasiwahi kuhusishwa na sakata hii.

Ahsante ya punda kwa kweli ni mateke, imetimika na nimeenda hadi tutakapokutana tena huko kwa kuzimu.

Kwa wanaonipenda mno familia, poleni na Mungu awe nanyi ninapowaacha. Mkumbuke kwamba msinizike bali mwili wangu uchomwe.

Kwaherini pia marafiki wangu feki,” akaandika.

Kisha akapatikana Agosti 10, 2023 iliyopita katika lojing’i moja ya Mji wa Nanyuki akiwa amejinyonga.

  • Tags

You can share this post!

Madaktari wataka afya iwe ajenda ya mazungumzo

Kamati kuchunguza ikiwa kuna madhara Worldcoin kumulika...

T L