• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 8:55 PM
Brown Mauzo atangaza kutengana na Vera Sidika

Brown Mauzo atangaza kutengana na Vera Sidika

NA MWANDISHI WETU

MWANAMUZIKI Brown Mauzo ametangaza kuvunjika kwa uhusiano kati yake na soshiolaiti Vera Sidika.

Kwenye ujumbe wake, Fredrick Mutinda almaarufu Brown Mauzo alisema kuwa walifikia uamuzi wa kutengana baada ya mazungumzo mengi ya kina na kuwaomba wafuasi wao kuwapa muda.

Mauzo ambaye aliungama kuwa mahusiano yake na Vera yalileta watoto wawili, Asia Brown na Ice Brown, walijifurahisha na kuunda kumbukumbu ambazo haziwezi kusahaulika.

“Ningependa kuwashukuru sana kwa upendo na umoja mliotuonyesha katika mahusiano yetu. Maneno yenu ya kutupa nguvu yalikuwa na umuhimu mwingi. Tunapofungua ukurasa huu upya maishani, tunawasihi mtuelewe na kuheshimu maisha yetu ya kibinafsi wakati huu,” akaandika.

Hapo awali, Vera alikuwa ameeleza kuwa wameachana na mpenziwe kisha kukataa madai ya kiki.

“Sio kila kitu maishani mwa mtu kinazunguka kiki. Watu huachana na maisha yakasonga mbele. Wengine huachana na kurudiana baada ya kusuluhisha vita vyao. Hivyo ndivyo maisha huwa, si nyororo,” akaandika.

Isitoshe, alitoa picha walizokuwa wamepigwa na Mauzo kisha kutomfuata katika mtandao wa kijamii wa Instagram.

Lebo ya ‘mke’ aliyokuwa ameweka wakati mahusiano yao yalikuwa yamenoga pia ilitolewa. Hapo ndipo wafuasi wao walianza kukisia kuwa hawakuwa pamoja.

Mauzo na Vera walianzia mahusiano yao mnamo 2020.

  • Tags

You can share this post!

SHINA LA UHAI: Hatari, tija za mwanamke kujifungua akiwa na...

Hisia mseto bei ya gesi ikishuka katika maeneo tofauti

T L