Na KNA
GAVANA kwale, Bw Salim Mvurya, ametaka kamati itakayochagua kikundi cha kuwakilisha kaunti hiyo kwenye mashindano ya kitaifa ya utamaduni, ifanye uamuzi wa haki.
Alisema hiyo itawezesha Kwale kuwakilishwa na kikundi bora zaidi kitakacholeta ushindi.
Makala ya mwaka huu yatafanyika Mombasa. Mwaka 2019 Kwale iliibuka ya pili kitaifa.
Mwaka 2020 hayakuwepo sababu ya janga la corona.