• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 5:55 AM
Huyu rafiki ataniambukiza tabia za usagaji?

Huyu rafiki ataniambukiza tabia za usagaji?

Nina rafiki na nimekuwa nikishangaa ni kwa nini sijamuona na mwanamume hata siku moja. Nimegundua ni mpenzi wa mwanamke mwenzake. Nachukia sana tabia hiyo na nahofia ataniambukiza. Nifanyeje?

Siku hizi kuna baadhi wanawake na pia wanaume walio katika uhusiano wa aina hiyo ingawa ni kinyume na maumbilr. Kama ni rafiki wa dhati, usivunje urafiki wenu kwa sababu hiyo. Muelewe tu naye pia aheshimu msimamo wako.

Mume anataka kuleta mtoto aliyezaa nje ili nimlelee, nishauri

Mume wangu alizaa mtoto na mpenzi wake wa awali kisha wakaachana. Mtoto huyo anaishi na nyanya yake. Anampenda sana na anafikiria kumchukua tuishi naye. Hiyo ni sawa?

Mume wako ndiye baba ya mtoto huyo kwa hivyo ana haki ya kuishi naye. Hata hivyo, uamuzi wake huo utategemea idhini ya mtoto huyo na iwapo pia wewe uko tayari kumlea kama wako.

Wanaume wengi kazini wananiandama na siko tayari kwa ndoa, nifanyeje?

Nina umri wa miaka 29. Kuna wanaume wengi tunaofanya kazi pamoja ambao wananitaka kimapenzi lakini siko tayari kwa sasa. Tafadhali nieleze jinsi ya kuwaepuka.

Hali hiyo inatarajiwa kwa mwanamke mchanga kama wewe. Mapenzi ni jambo la hiari si lazima. Waambie wazi wanaokutaka kwamba hujawa tayari kwa jambo hilo.

Mwanamume rafiki ya mume wangu anashinda akinipigia simu eti ataka tukutane ilhali ameoa

Mwanamume rafiki ya mume wangu amekuwa akinipigia simu akitaka tuonane. Ana familia pia na sijui ni kitu gani anataka kuniambia ambacho hawezi kuniambia kwa simu. Nifanye nini?

Hizo ni dalili kwamba mwanamume huyo anakutaka kimapenzi na ndiyo sababu anasisitiza muonane ana kwa ana. Kama hutaki kuharibu ndoa yako, usikubali wito wake.

  • Tags

You can share this post!

Wawili wafariki ubomoaji ukichacha mjini Mavoko

Vidosho kutoka Uganda, Tanzania wafurika Rift Valley...

T L