• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 5:01 PM
Kalonzo amewekwa chini ya kizuizi cha nyumbani – Wandayi

Kalonzo amewekwa chini ya kizuizi cha nyumbani – Wandayi

NA STEVE OTIENO

KIONGOZI wa Wiper Kalonzo Musyoka amewekwa chini ya kizuizi cha nyumbani tangu Jumanne wiki hii, amesema Mbunge wa Ugunja Opiyo Wandayi.

Akiwa na Katibu Mkuu wa Jubilee Jeremiah Kioni nyumbani kwake Kalonzo mtaani Karen, Bw Wandayi ambaye ni Kiongozi wa Wachache katika Bunge la Kitaifa amesema Makamu wa Rais wa zamani hajaruhusiwa kuondoka kwake tangu siku hiyo.

Vile vile amesema magari ya wanadiplomasia wa Umoja wa Mataifa (UN), Amerika, Muungano wa Ulaya (EU), na mataifa mengine, yameonekana yakitoka katika makazi hayo leo Ijumaa.

“Hatujui ni kwa nini magari hayo yalikuwa nyumbani kwake Bw Musyoka,” amesema Bw Wandayi.

  • Tags

You can share this post!

Mjane wa Kihindi apinga mwanamke wa Kiafrika kurithi mali

Polisi wawanyanyasa wanahabari wakifuatilia matukio...

T L