Na ANTHONY KITIMO
MAMLAKA ya Ukusanyaji Ushuru ya Kenya (KRA) imepanga kupiga mnada mizigo ambayo imechelewa kuchukuliwa katika Bandari ya Mombasa kuanzia leo Jumatano.
Mizigo hiyo inajumuisha vifaa vya kielektroniki, magari, vyombo vya nyumbani miongoni mwa mingine ambayo imekaa bandarini kwa muda mrefu kupita kiasi.
Mratibu wa KRA anayesimamia maeneo ya kusini mwa nchi, Bw Joseph Tonui, alithibitisha kuwa baadhi ya mizigo itakayopigwa mnada ilikuwa imenuiwa kusafirishwa hadi nchi nyingine za nje.