• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 4:42 PM
Maajenti 60 wa Old Mutual watuzwa kwa kazi nzuri

Maajenti 60 wa Old Mutual watuzwa kwa kazi nzuri

NA LAWRENCE ONGARO

KAMPUNI ya bima ya Old Mutual imejitolea kuwahamasisha maajenti kuendelea kuwa wakakamavu kazini.

Mkurugenzi wa Old Mutual Arthur Oginga, amewatia shime maajenti waendelee kufanya kazi kwa uadilifu.

“Maajenti wanafanya kazi nzuri kuboresha mauzo na kuiletea kampuni faida kubwa kila mwaka,” alieleza mkurugenzi huyo.

Maajenti wapatao 60 walitunukiwa zawadi huku wengi wakipangiwa kusafiri hadi visiwani Zanzibar na nchini Namibia kisha baadaye wazuru Amerika.

Baadhi yao nao watafanya ziara za nchini na za nchi za ng’ambo.

Afisa mwingine wa Old Mutual Calvince Onduru aliwapongeza maajenti hao waliopokea tuzo na kuwahimiza waendelee kujitolea  ili kupiga hatua zaidi.

Old Mutual imehudumia wateja wake kwa takribani miaka 100 tangu kubuniwa na ambao wako katika mataifa ya Uganda, Rwanda, Sudan Kusini, Tanzania na Kenya.

Mkurugenzi wa bima katika shirika hilo Bw Japheth Ogallo alipongeza kazi nzuri inayotekelezwa na maajenti hao akisisitiza wanatambua kazi nzuri wanayotekeleza.

“Tunaelewa kuwa maajenti wetu wanafanya kazi nzuri na kwa hivyo tutaendelea kushirikiana nao ili kuwapa motisha zaidi,” alisema Bw Ogallo.

  • Tags

You can share this post!

Baadhi ya vyanzo vya furaha maishani mwako

Benki ya KCB yapiga jeki matayarisho ya Safari Rally kwa...

T L