• Nairobi
  • Last Updated May 11th, 2024 9:55 AM
Mhadhiri katika chuo kikuu ashtakiwa kwa kuwadhulumu watoto kimapenzi

Mhadhiri katika chuo kikuu ashtakiwa kwa kuwadhulumu watoto kimapenzi

NA RICHARD MUNGUTI

RAIA wa Amerika aliyeingia nchini kufanya kazi ya kuhubiri na kufunza katika chuo kikuu kimojawapo cha kibinafsi ameshtakiwa kwa kuwadhulumu watoto kimapenzi.

Anatakiwa nchini Amerika kujibu mashtaka ya dhuluma za watoto.

Aliposhtakiwa mbele ya hakimu mwandamizi katika mahakama ya Milimani Robinson Ondieki, Bw Joseph Williams Black JR aliye na umri wa miaka 64 alikana mashtaka kusambaza katika mitandao ya Microsoft na Skype video za watoto walio na umri wa miaka 14 wakifanya ngono.

Pia afisa wa polisi kutoka kitengo cha kutetea haki za watoto katika Idara ya Kupeleleza Makosa ya Jinai (DCI) Wycliffe Jefwa alitoa picha 14 za watoto wakiwa uchi wa mnyama.

Mkufunzi huyo alikamatwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA).

Alipokamatwa, polisi walitoa katika tarakilishi yake video za ngono alizokuwa akisambaza katika mitandao ya Microsoft na Skype.

Polisi walihofu ataenedeleza uovu huo.

Picha alizokuwa nazo za watoto wakiwa uchi ni za watoto wazungu ambao hawajulikani asili yao.

Alishtakiwa katika Mahakama ya Milimani jijini Nairobi.

Alikana mashtaka kisha Bw Jefwa akawasilisha ushahidi dhidi ya William wa video na picha 14 za watoto wa umri kati ya miaka 14 ma 15 wakiwa uchi wa mnyama.

Bw Jefwa alieleza mahakama kwamba polisi walivamia makazi ya Williams katika eneo la Riruta, Nairobi ya Bishop Makarios Seminary na kupata picha hizo.

Bw Jefwa alieleza mahakama kuwa walinasa picha na video nyingine katika kipakatalishi cha mshtakiwa alipokuwa akijaribu kutoroka nchini.

“Polisi walipokea habari kwamba mshtakiwa anayetakiwa nchini Amerika kushtakiwa kwa kukandamiza haki za watoto alikuwa anaishi Kenya,” Bw Jefwa alimweleza hakimu.

Baadaye, hakimu alifahamishwa polisi walivamia makazi ya mshtakiwa na kupata ushahidi wa dhuluma za kimapenzi dhidi ya watoto.

William alishtakiwa wiki tatu baada ya raia mwingine wa Amerika Terry Ray Krieger kushtakiwa katika mahakama ya Mavoko katika Kaunti ya Machakos kwa dhuluma za kimapenzi dhidi ya watoto.

Pia wiki iliyopita raia wa Uholanzi Jan Int Veld almaarufu Dad Ok almaarufu Teacher Jan almaarufu Mzungu, alishtakiwa kwa kuwadhulumu kimapenzi watoto katika Kaunti ya Uasin Gishu.

  • Tags

You can share this post!

Wanaume wa kupenda ndogondogo watiwa majaribuni kwa...

Kuppet yalia kucheleweshwa kwa pesa za walimu...

T L