Na RICHARD MUNGUTI
MWANAUME aliyedai fidia ya Sh1.9 milioni kwa njia ya vitisho ameshtakiwa.
Benson Gathua ameshtakiwa kushirikiana na watu wengine ambao hawajafikishwa kortini kwa kumtishia maisha Margaret Wambui endapo hatawapa Sh1.9 milioni.
Gathua alishtakiwa kudai pesa hizo kati ya Septemba 13, 2020 na Mei 1, 2023 katika mtaa wa Utawala, Kaunti Ndogo ya Njiru, Nairobi.
Hakimu mkuu Francis Kyambia alifahamishwa Wambui alipokea kifurushi kilichokuwa na vifaa vya uchawi.
Kiongozi wa mashtaka alisema mlalamishi alipokea vitisho na kiwango cha pesa alichoitishwa kikapunguzwa hadi Sh1.5 milioni.
Mahakama ilimwachilia mshtakiwa kwa dhamana ya Sh400, 000.
Kesi itatajwa Juni 15, 2023 na kuanza kusikizwa Septemba15, 2023.