• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:33 PM
Mshukiwa wa ujambazi ashtakiwa kwa kudai fidia ya Sh1.9 milioni

Mshukiwa wa ujambazi ashtakiwa kwa kudai fidia ya Sh1.9 milioni

Na RICHARD MUNGUTI

MWANAUME aliyedai fidia ya Sh1.9 milioni kwa njia ya vitisho ameshtakiwa.

Benson Gathua ameshtakiwa kushirikiana na watu wengine ambao hawajafikishwa kortini kwa kumtishia maisha Margaret Wambui endapo hatawapa Sh1.9 milioni.

Gathua alishtakiwa kudai pesa hizo kati ya Septemba 13, 2020 na Mei 1, 2023 katika mtaa wa Utawala, Kaunti Ndogo ya Njiru, Nairobi.

Hakimu mkuu Francis Kyambia alifahamishwa Wambui alipokea kifurushi kilichokuwa na vifaa vya uchawi.

Kiongozi wa mashtaka alisema mlalamishi alipokea vitisho na kiwango cha pesa alichoitishwa kikapunguzwa hadi Sh1.5 milioni.

Mahakama ilimwachilia mshtakiwa kwa dhamana ya Sh400, 000.

Kesi itatajwa Juni 15, 2023 na kuanza kusikizwa Septemba15, 2023.

  • Tags

You can share this post!

Mzee ashtakiwa kwa ulaghai wa shamba la mabilioni Nairobi

SIHA NA LISHE: Tunda la chenza

T L