• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 7:05 PM
Mwanamume mpenzi wangu alichovya nje nikamtema, sasa nahisi upweke

Mwanamume mpenzi wangu alichovya nje nikamtema, sasa nahisi upweke

SHANGAZI;

Nilimuacha mpenzi wangu nilipogundua ananicheza na mwanamke rafiki yangu. Nimeamua kutafuta mwingine lakini imekuwa vigumu kwa sababu bado nampenda.

Mapenzi ni suala la moyoni. Unaungama kuwa umeshindwa kutafuta mpenzi mwingine sababu bado unampenda uliyemuacha, licha yake kutokuwa mwaminifu kwako. Fuata moyo wako. Msamehe kisha mrudiane.

Anatosha kuwa mke lakini ni sumbua sana

Nimepata mpenzi baada ya kutafuta kwa miaka kadhaa. Mapenzi yetu ni ya dhati na anatosha kuwa mke wangu. Tatizo ni kuwa ana wivu sana. Nisipokuwa naye husumbua sana kwa simu akifikiri nina mwingine.

Wivu wa mpenzi wako unatokana na mapenzi yake kwako. Kama kuna mambo anayohitaji kujua kupitia kwa simu ili kuondoa wasiwasi wake msipokuwa pamoja, ni vyema umuelewe.

Ex bado ananitaka licha ya kuwa mume wa mtu

Niligundua majuzi kuwa mpenzi wangu ana wanawake wengine, nikamuacha. Wangu wa zamani anataka turudiane ingawa ameoa. Nampenda lakini sitaki kuharibu ndoa yake.

Jihadhari na wanaume wa kukutumia vibaya. Jiulize ni kwanini mwanamume huyo alikuacha akaoa mwanamke mwingine. Pili, ameoa na hawezi kuwa mume wako. Mbona usitafute wako badala ya kuwa mpango wa kando?

 

Jombi anaeneza uvumi kuniharibia penzi

Nina umri wa miaka 27. Kuna mwanamume fulani aliyenitaka lakini sikukubali. Sasa ameanza kueneza uvumi eti sisi ni wapenzi. Nina mpenzi na nahofia habari hizo zikimfikia ataleta shida.

Nia ya mwanamume huyo ni kuharibu uhusiano wenu kwa uvumi huo. Anatarajia ukimfikia mpenzi wako akulaumu kwa kutokuwa mwaminifu kwake. Ni muhimu umwambie mapema.

  • Tags

You can share this post!

Waumini wabaki na mshtuko kanisa la thamani ya Sh650...

Uhuru, mamake wavunja kimya na kumuomboleza shujaa wa Mau...

T L