• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 6:07 PM
Mwitaliano ashtakiwa kuiba teksi

Mwitaliano ashtakiwa kuiba teksi

Na RICHARD MUNGUTI

MWITALIANO aliyekiri Ijumaa aliiba teksi kutoka Nairobi na kutoroka nayo hadi Mombasa alikuwa na bahati ya mtende aliposamehewa na mlalamishi kisha akaitamatisha kesi dhidi ya mgeni huyo.

Alipofikishwa kortini, Maurizio Monticelli alikiri shtaka la kuiba gari la Bw Amos Kalawa.Monticelli alikubali mbele ya hakimu mkazi Bw William Tulel kwamba aliiba gari hilo la Bw Kalawa ya thamani ya Sh1.1milioni.Aliposomewa mashtaka na hakimu na kuulizwa ikiwa anakubali au anakataa Monticelli alitikia mara mbili akisema, “Nikweli niliiba.Nikweli niliiba.”

Kabla ya hakimu kupokea maelezo jinsi wizi ulitekelezwa Bw Kalama alisimama kizimbani na kueleza mahakama nia yake ya kutamatisha kesi hiyo.“Mheshimiwa niko na jambo la kueleza hii mahakama,” Bw Kalawa alisema.Bw Tulel alimwuliza mlalamishi jambo alilokuwa anataka kuambia mahakama.

Mlalamishi alijibu nakusema “Sitaki kuendelea na hii kesi. Nilipata gari langu na nimeridhika polisi walitekeleza kazi yao ipasavyo. Nimemsamehe mshtakiwa. Tamatisha kesi dhidi yake.”Mshtakiwa alikabiliwa na shtaka la badala la kupatikana na gari mjini Mombasa akijua imeibwa ama kupatikana kwa njia isiyo halali.

Gari hilo lilipatikana Shanzu mjini Mombasa.Baada ya kuiba teksi hiyo Monticelli alimwajiri dereva awe akiendesha kazi ya teksi Bamburi na Shanzu mjini Mombasa.Mshtakiwa alikuwa amemkodisha tesksi hiyo kwa matembezi yake akiwa ziarani Nairobi.

Mshtakiwa alimtuma dereva wa teksi hiyo ya Bw Kalama kumnunulia sigara kisha akatoroka nayo.Dereva wa teksi hiyo aliyeacha gari ikinguruma akienda kumnunulia sigara hakuamini macho yake kwa vile hakuipata gari lake.

 

  • Tags

You can share this post!

Wauzaji pombe Nakuru waonywa

Aliyejaribu kuua polisi kukaa gereza la viwandani