Na RICHARD MUNGUTI
NAIROBI itapata Gavana mpya baada ya Mahakama ya Rufaa kuamuru aapishwe mara moja.
Wakiamuru Bi Anne Kananu aapishwe achukue hatamu za uongozi wa kaunti ya Nairobi Majaji Wanjiru Karanja, Jamila Mohammed na Jessie Lesiit walisema suala la kuapishwa kwake halikulalamikiwa katika kesi iliyowasilishwa katika mahakama kuu na mwanaharakati Okiya Omtatah
Bw Kananu aliyekuwa ameteuliwa kuwa Naibu wa Gavana Mike Sonko alipata changamoto baada ya Jaji Antony Mrima kuamuru asitwae hatamu za uongozi. Jaji Mrima alihoji uhalali wa Bw Sonko kumteua Bi Kananu.
Kuapishwa kwa Bi Kananu kulipingwa na majaji hao watatu wakasema “suala la kuapishwa halikuwa mojawapo ya tetezi za rufaa hiyo. ”Bw Omtatah na Bw Sonko waliwasilisha kesi kupinga kuapishwa kwa Bi Kananu aliyekuwa ameajiriwa katika idara ya kushughulikia masuala dharura na pia sekta ya maji.
Kabla ya Bi Kananu kutwaa hatamu za ugavana Nairobi, spika wa bunge la kaunti ya Nairobi na mbunge wa zamani Makadara Benson Mutura ndiye alikuwa anahudumu katika wadhifa huo.
Gavana huyu mpya atakuwa anafanyakazi na Meja Jenerali Mohamed Badi aliyeteuliwa na Rais Uhuru Kenyatta kulainisha utenda kazi katika kaunti hii nambari 47.