NA OSCAR KAKAI
Panzi wamevamia Kaunti Ndogo ya Pokot ya Kati, Kaunti ya Pokot Magharibi kutokana na kiangazi ambacho kimesababisha wadudu hao kutaga mayai, kuzaa na kukua.
Panzi hao wamevamia mashamba katika eneo hilo kame na kuharibu mazao, nyasi na mimea na kutishia utoshelevu wa chakula katika eneo hilo.
Wadudu hao wamevamia maeneo ya wadi za Weiwei na Lomut katika eneobunge la Sigor na kuharibu mimea.
Wakazi wanaitaka serikali kukabili wadudu hao ambao wamekuwepo kwa wiki tatu sasa