• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 10:50 AM
Bondia Wanyonyi adhihirisha Kenya imara kwa kumtandika Mandonga ‘mtu kazi’   

Bondia Wanyonyi adhihirisha Kenya imara kwa kumtandika Mandonga ‘mtu kazi’  

NA MWANGI MUIRURI

BONDIA Daniel Wanyonyi amedhihirisha kuwa Kenya ni imara katika ndondi, baada ya kumwangushia mwenzake Mtanzania Karim Mandonga maarufu kama ‘Mtu Kazi’, mangumi yaliyomvunia ushindi mnamo Julai 22, 2023.

Mandonga aliingia ukumbini ‘akibeba mdomo mkubwa’ jinsi angemrambisha sakafu shujaa Wanyonyi, lakini hali ikaishia kinyume aliponyeshewa makonde mazitomazito.

Isipokuwa ni bahati ya mtende, Mandonga angejipata katika hali mbaya sana kwa kuwa aliangushwa katika raundi ya sita na pia ya kumi na mashabiki walikuwa wanamuomba refa wa uhasama huo atamatishe mechi kumwokoa.

Mandonga alikuwa amemshinda kwa wembamba wa uzi Januari 14, 2023 katika ukumbi wa KICC, jijini Nairobi walipomenyana, Wanyonyi wakati huo akisema alikuwa na shida ya kiufundi ambayo aliahidi kurekebisha na kisha akaomba warejelee makonde baadaye.

Katika awamu ya kwanza, Bw Wanyonyi alikataa kuamkia pambano hilo katika raundi ya sita na ndipo Mandonga akapewa ushindi kwa kubakia amesimama peke yake jukwaani.

Lakini mambo yaligeuka tofauti katika ukumbi wa Sarit ambapo Wanyonyi alionyesha ustadi wa juu alipomnyooshea mikono ya uzito kutoka kila anwani ya angani.

Hatimaye, waamuzi waliamua kwamba kwa wingi wa pointi Bw Wanyonyi alikuwa amemramba Bw Mandonga ambaye jukwaani alikuwa amezima bwebwe zake za kawaida.

 

[email protected]

 

 

  • Tags

You can share this post!

Panzi wazua hofu wakiharibu mimea

Mwenyekiti wa Azimio Nakuru alalamikia waandamanaji kuiba...

aaronmalcolm48