• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 7:55 PM
Pasta amenitunga mimba kisha akaniruka!

Pasta amenitunga mimba kisha akaniruka!

SHANGAZI;

Nimekuwa na uhusiano wa kimapenzi na pasta wa kanisa langu. Nina mimba yake lakini amenikana. Hujifanya matakatifu sana na hata nikiambia watu hakuna anayeweza kuniamini. Nifanyeje?

Pasta pia ni binadamu na anaweza kunaswa na kutumiwa na shetani. Sielewi uhusiano wenu ulianzaje hadi ukafikia hapo. Unafaa kujilaumu kwa matokeo hayo pia. Sasa amekuhepa na itabidi ubebe mzigo huo.

Niliyemtaka kwa miaka 2 sasa amenijia lakini tayari nimepata mwingine

Mwanamke ambaye nimekuwa nikimtaka kwa miaka miwili alinitumia ujumbe juzi akaniambia yuko tayari kuwa mpenzi wangu. Nimepata mwingine ambaye nampenda hata zaidi. Nifanyeje?

Sidhani unahitaji ushauri wangu ili kuamua kuhusu jambo hilo. Kama umepata ambaye umetosheka kuwa ndiye chaguo la moyo wako, itabidi umwambie huyo mwingine ingawa uamuzi huo utamvunja moyo.

Sijawahi kupendana na mwanamke na sina hisia

Nina umri wa miaka 31 na sijawahi kuwa na mpenzi maishani kwa kuwa sina hisia zozote kwa wanawake. Marafiki zangu, wakiwemo wanawake, wamekuwa wakinicheka kuhusu hali yangu hiyo. Nifanyeje?

Una sababu ya kuwa na wasiwasi kwani hiyo si hali ya kawaida. Katika umri wako huo unafaa kuwa na mpenzi na pia marafiki wengine wanawake. Tafuta mtaalamu wa afya ya uzazi uone kama atakusaidia.

Sitaki kuolewa, kuzaa, nataka mtu anipe raha

Nina umri wa miaka 30. Nimeamua sitaki mpenzi na sitaolewa kwa sababu siwezi kumwamini mwanamume yeyote. Lakini nahitaji wa kunipa raha tu na sitaki kupata mimba. Waonaje?

Wewe sasa ni mtu mzima na una haki ya kuishi maisha unayotaka. Umeamua kuishi hivyo kwa sababu zako. Kama unahitaji mwanamume na hutaki mimba, basi itabidi mtumie kinga.

  • Tags

You can share this post!

Isaac Mwaura ateuliwa Msemaji wa Serikali

Rais Ruto aendelea kummegea Mudavadi tonge serikalini

T L