• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 2:35 PM
Polisi wapata afueni kwenye kesi ya mauaji

Polisi wapata afueni kwenye kesi ya mauaji

NA PHILIP MUYANGA MAHAKAMA Kuu imezima kwa muda uamuzi wa kuwashtaki maafisa watano wa polisi kwa madai ya kumuua mhudumu wa bodaboda Likoni wakitekeleza masharti dhidi ya Covid-19.

Jaji Olga Sewe, alitoa agizo hilo alipokubali ombi la maafisa hao la maagizo kadha ikiwemo uamuzi kwamba hawakuwa na nia yoyote iliyopangwa kuhusu kisa kilichosababisha kifo cha Hamisi Juma.

Jaji alisema uamuzi aliotoa utadumu hadi wakati ombi la maafisa hao litasikizwa na kuamuliwa. Hamisi alidaiwa kuuawa na polisi mnamo Machi, 2020.

  • Tags

You can share this post!

Azimio wamtaka Rigathi akae kando ya mazungumzo

Maambukizi ya Ukimwi yapungua nchini- NSDCC

T L