• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 6:50 AM
Ruto akana kumwekea mtego Gachagua

Ruto akana kumwekea mtego Gachagua

NA VITALIS KIMUTAI

RAIS William Ruto jana Jumapili alikanusha madai kuwa anamtega naibu wake Rigathi Gachagua.

Alisema hatua ya kumpa naibu wake majukumu ya kukabiliana na wahuni katika sekta ya kilimo si mtego kama inavyodhaniwa.

“Sijamwekea mtego naibu wangu (Bw Gachagua). Yeye akifeli, mimi pia nitakuwa nimefeli,” akasema Dkt Ruto wakati wa maombi ya kutoa shukrani katika uwanja wa michezo wa Bomet.

Siku ya Jumamosi, Taifa Leo iliripoti hisia za wachanganuzi waliohisi kuwa majukumu aliyopewa Bw Gachagua huenda yakawa mtego kwake.

Wadadisi wanasema kuwa, majukumu hayo mazito huenda yakamponza Bw Gachagua kwa kumfanya kupoteza umaarufu kufikia 2027.

Majukumu aliyopewa Bw Gahcagua kama kusafisha Mto Nairobi na kukabiliana na wahuni wanaoumiza wakulima, ni sawa na yale aliyopewa aliyekuwa waziri Mkuu Raila Odinga wakati wa serikali ya ‘nusu-mkate’.

Kubomoa majumba ya watu ili kujenga barabara za kisasa pamoja na kuwafurusha wakazi kutoka Msitu wa Mau, ni mambo yaliyomkosesha umaarufu Bw Odinga wakati huo.

Lakini jana Jumapili, Dkt Ruto alisema marekebisho katika sekta za kahawa na majani chai, yataendelezwa na Bw Gachagua ili kuwawezesha wakulima kula jasho lao.

  • Tags

You can share this post!

Maswali yazuka kuhusu aliko ‘Sultani’ Joho

Barcelona watandika Real Madrid na kutawazwa wafalme wa...

T L