• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 2:00 PM
SHANGAZI AKUJIBU: Mume wangu amefutwa kazi na haniambii, je, nimuulize?

SHANGAZI AKUJIBU: Mume wangu amefutwa kazi na haniambii, je, nimuulize?

Nimepata habari kuwa mume wangu aliachishwa kazi miezi miwili iliyopita na nimethibitisha kupitia kwa bosi wake. Lakini hajaniambia na amekuwa akiondoka kila asubuhi kama kawaida. Nifanye nini?

Ninaamini mume wako amefanya hivyo kwa makusudi. Anajua tukio hilo linaweza kuzua hofu nyumbani kwa sababu mnamtegemea kwa mahitaji yenu. Huenda ameamua kutafuta kazi nyingine kimya kimya. Usimuulize chochote hadi atakapokwambia yeye mwenyewe.

Fukara mwenye penzi na tajiri asiyejua kupenda, niolewe na yupi?

Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 29. Ninatafuta mchumba. Tafadhali niambie aliye bora kati ya hawa mawili. Mume mwenye pesa bila mapenzi ya dhati ama mume mwenye mapenzi ya dhati bila pesa?

Hakuna chochote cha kulinganishwa na mapenzi ya dhati katika ndoa. Mapenzi ya dhati ndiyo nguzo kuu katika ndoa kwa sababu yanawafunga wawili pamoja hadi kifo kuwatenganisha. Pesa huisha.

Nampenda, shida ni mamake

Nina umri wa miaka 32. Sina mpenzi ingawa kuna mwanamume anayenipenda. Nampenda pia lakini shida ni mama yake. Nimeona dalili kwamba hanipendi. Nahitaji ushauri wako.

Naelewa unataka kuwa na uhusiano mwema na jamaa wa mpenzi wako hasa ukiolewa katika familia hiyo. Lakini huwezi kuvunja uhusiano wako eti kwa sababu mama ya mpenzi wako anakuchukia bila sababu. Maisha ni yako na mpenzi wako.

Mke ametoboa siri mtoto si wangu, nitafanyeje?

Mke wangu alijifungua mtoto wetu wa kwanza mwezi uliopita. Nimekuwa nikishuku iwapo mtoto huyo ni wangu na hatimaye juzi aliungama amekuwa na mpango wa kando. Nifanyeje?

Hatimaye umethibitisha wasiwasi wako. Kwamba mke wako alikucheza na mwanamume mwingine na mtoto si wako. Utaamua mwenyewe kama utamuacha ama utamsamehe na kumkubali mtoto huyo.

  • Tags

You can share this post!

Munya sasa akujiwa baada ya Oparanya

Nikabidhiwe jeshi langu, Jenerali Muhoozi aambia babake,...

T L