BARNABAS BII Na ANTHONY KITIMO
SHEHENA ya kwanza ya mahindi ya manjano inatarajiwa kuingia nchini leo Jumapili.
Japo meli hiyo iliyobeba zaidi ya tani 42,000 za mahindi ya manjano inatarajiwa kufika nchini, hakuna dalili ya bei ya unga kushuka hivi karibuni.
Wasagaji mahindi wasema hiyo haitaleta tofauti yoyote kwani mahindi ya manjano hutumiwa zaidi kutengeneza vyakula hasa vya mifugo.